Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jan 28, 2011

ZIARA YANGU HOLLYWOOD(LOS ANGELES)

Nimetembelea Hollywood hapa UNIVERSAL STUDIOS kuona mambo mbalimbali ya filamu za hapa hollywood,hii inakuwa mara yangu ya pili kufika hapa.


Hawa ni wasanii walioko maeneo haya ya UNIVERSAL STUDIOS.





Hollywood ndio hiyo,,,


Hii ni SOUND STAGE 12,ndiko kunakorekodiwa tv shows au scene za ndani katika movie


Nikishangaa kwa 3D namna alivyotengenezwa yule nyani wa KING KONG


Kwa wale wanaojua mambo ya blue au green screen mnaelewa kazi yake hiyo,hapo unaweza kushoot alafu katika editing ukawekwa sehemu yoyote.


katika movie movie wengi hushangaa magari yanawezaje kupaa na kulipuka?basi huu ndio utaalamu wao.hapa kabla


Director akisema action basi hali huwa hivi...





kisha hurudishwa sehemu yake kwa namna hii


Jinsi wanavyotengeneza mvua


Bomba hili linatoa maji kwa juu kama mvua ambapo


Jinsi wanavyotengeneza mafuriko ya mvua,hufungulia mabomba makubwa pembeni ambayo huleta maji kwa kasi kama unavyoona

Maji yakipungua na kuingia katika mitaro ya kutengenezwa

Hii ni mfano wa meli ambazo hutumiwa shooting na baadae katika editing na special effect hufanya meli kuonekana kubwa kulingana na saizi waliyokusudia,hili unaweza kuliona katika TITANIC MOVIE

Jinsi ya kutengeneza maporomoko ni kama unavyoona hayo yote yanaendeshwa na umeme

Jan 23, 2011

The great ndani ya club MILLENIUM..WASHINGTON DC

















SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KWA DJ LUKE JOE ...ASANTE SANA KWA MWALIKO KAKA

THE GREAT AKUTANA NA SAMUEL MALONJA

Nikiwa hapa Washington Dc nimekutana na rafiki yangu wa siku nyingi Mr.Samuel Malonja,huyu kabla ya kuja huku ndiye alikuwa akitengeneza soundtrack za movie zangu lakini pia nimewai kupiga nae mziki wa gospel kanisani katika kwaya ya NEEMA GOSPEL(A.I.C.T-CHANG'OMBE).Alinialika kwake na baada ya kufika akatoa magitaa ili tujikumbushie...basi tukaporomosha ziki kari la kimya kimya...

Samuel na mimi

Akishangaa jinsi ninavyoshusha vipande

mmh namimi kidogo nikimshangaa vitu anavyoshusha

kwa pamoja tukawakilisha

Jan 21, 2011

KANUMBA THE GREAT FILMS present..........

Hata nikiwa nje ya nchi lakini ofisini kwangu kazi zinaendelea kama kawaida na mwezi huu kwa kuanza mwaka naanza na hii...''DECEPTION''sina haja ya kuongea mengi hata kwa picha tu upekee na utofauti waweza tizama katika picha kwamba ni kivingine,,naanza kwa mbio mwaka huu,,kaa mkao wa tayari soon inakuwa mtaani,,,mashabiki wa kweli na wazalendo hununua copy original na si feki,lakini pia hawaazimani bali kila mtu hununua ya kwake tena original.''Mkataa kwao ni mtumwa''.....''Mcheza kwao hutunzwa''......''Tusitukuze vya nje na kudharau vyetu maana upendo wa dhati huanzia nyumbani na si ugenini,tujikubari sisi wenyewe kwa kupeana mioyo na kushauriana kwa njia na nia njema bila kutukanana wala kupondana maana lengo letu ni zuri kwa jamii....PATA NAKALA YAKO SASA.... poster lake....

Kanumba na Rose Ndauka ktk movie hii wakiwa katika mapozi tofauti











Jan 20, 2011

THE GREAT IN NEW YORK....

Leo nimetembelea New york city kununua vifaa vya production katika kampuni yangu...nimetembelea duka moja kubwa na maarufu kwa vifaa vyote vya movie production na sound linaloitwa B&H. Nikitizama taa nzuri kwa production

Nikiwa makini kuchagua ili mashabiki wangu wa ukweli niwe nawapa vitu vyenye quality

Hapa ni sehemu za BOOM MIC pesa yako tu hapo kuna kila aina ya mic kwa ajili ya production napo nilichukua mojawapo ili sauti iwe nzuri katika movie zangu.

Hizi husaidia kuzuia upepo wakati wa shooting

Duka hili lina kila kitu hadi drums,hapa nikijaribu kidogo ili siku nikija kuwa mwanamziki nipite tena hapa.

Vinanda na spika zake vipo







Japo camera tayari ninayo tena nzuri tu ila nilipita hapa sehemu zinapouzwa camera kuosha macho kidogo kwa sababu sikuitaji kitu hapa.



Crain zipo za aina mbalimbali

Duka lenyewe linavyoonekana kwa nje katika mitaa ya NEW YORK.

Kwa vile vifaa nilivyoweza kubeba kwa mikono nilibeba vingine nilipakia,hii ni kuonesha kuwa kwa mwaka 2011 mashabiki wangu nimejipanga vizuri kukonga nyoyo..

Jan 19, 2011

WAKATI BONGO TWALIA NA JOTO WENZETU HUKU WALIA NA SNOW....

Hii imemwagika leoleo......Washington dc na sehemu zingine...





Mzee Yusuph Kalala akikwangua barafu katika gari

The great na Mzee Kalala kwa pamoja tunawakilisha..

Jan 18, 2011

BERRY BLACK IN OSLO

Jan 17, 2011

THE GREAT IN U.S.A

The great kwa sasa niko Marekani kwa mapumziko mafupi na katika pitapita nikakutana na dada yetu mbunifu maarufu wa mavazi nchini Asia Idarus maeneo ya Washington akiwa na mmewe tukapata picha ya pamoja. Asia,Hamsini,na The great in America

Hamsini,Dada Sharifa Kalala na The great..