The great niliamua kumtembelea hotelini alipofikia mwanamziki mkongwe kutoka CONGO ambae pia ni muasisi wa wenge musica bcbg kabla ya kujiengua na kuunda kundi lake la wenge tonya tonya,nikaamua kumtoa kidogo kwenda sehemu kadhaa kama...

Hapa ilikuwa katika studio za GRM PRODUCTION tukipiga picha za kumbukumbu ambapo pia video camera ilikuwa ikishoot ambayo nayo nilimpatia aondoke nayo.

Hapa akiwa na mkurugenzi wa GRM PRODUCTION Nd.G.Makupa ambae zoezo zima la picha aliliongoza yeye hapo studio.

Hapa nikimkabithi zawadi ya simu mpya kama kumbukumbu pindi afikapo kwao

mdau,adolphe,the great na G.Makupa kwa pamoja baada ya kumpatia zawadi ya simu Adolphe

Hapa nikimkabithi zawadi ya movie yangu mpya inayosumbua kisawaswa THIS IS IT 1&2 ambayo aliomba maana kwao bado haijafika

kwa pamoja tukiimba wimbo wake wa VOYAGE alioutunga na kuimba zamani akiwa na wenge bcbg akiwa na JB MPIANA,BLAISE BULA,WERRASON,AIMELLA,ALLAIN MPELLA,ALLAN MAKABA,nk.

aliniomba kabla ya kumkabithi movie zangu nisaini kwanza nami nikafanya hivyo

Nae pia baada ya kumrudisha hotelini alinipa zawadi ya albam yake mpya aliyoimba na KOFFI OLOMIDE(audio na dvd)inayoitwa SUSPENSION

Hii ni moja ya picha tulizopiga na kuzikuza na kutoa picha kubwa2 ambazo kwa upande wake alisema anaenda kupamba nyumbani kwake lakini mimi nilisema ntaweka ofisini kwangu ambapo nilimpitisha akapaona.