Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Sep 10, 2010

MORE THAN PAIN IKO MADUKANI SASA PATA NAKALA YAKO ORIGINAL

Filam yangu mpya ya MORE THAN PAIN iko madukani plz pata nakala yako original na si feki,k tuwe wazalendo kwa kupenda kazi zetu za nyumbani.movie hii nimemshirikisha LISA JENSEN na ROSE NDAUKA Postar lake

Sep 8, 2010

BAADA YA KAZI NZITO YA KUSHOOT,THE GREAT OFISINI.

Baada ya mda wote toka asubuhi mpaka jioni kuwa location nikishoot usiku baada ya hapo naingia ofisini kwangu kukagua kile nilichokuwa nafanya siku nzima kama kiko katika ubora niliokusudia ili kazi ianze ku haririwa(editing) The great nikipreview scene nilizoshoot katika monitor za computer yangu aina ya MAC-G5

Kwa umakini nikikagua

Kuna wakati inabidi nitumie camera kuingiza material ktk computer...

THE GREAT KATIKA UNCLE JJ NA WANANGU

Me sisemi mtaona wenyewe

Farid Uwezo akihakikisha anapata picha sawia

The great nikiwai bafuni

Jenifa akichuma mboga mboga

Uncle jj na patriq

Vituko vya huyu mtoto ni vingi mno katika hii movie

Scene hii akiwachimba mkwara watoto wenzake

Uncle jj akisisitiza jambo

Jenifa akaona isiwe tabu wacha nami nijaribu hajui mtaka vyote hukosa vyote

Wakati fulani anakuwa mshauri mzuri kwa wenzie kama unavyoona

The great a.k.a uncle jj nikichimba mkwara kwa Jenifa

Farid Wezi au Uwezo ndie camera man wangu

Sep 7, 2010

KANUMBA THE GREAT FILM MZIGONI.

The great nimeanza kuandaa kazi yangu mpya iitwayo UNCLE JJ nikiwa na wanangu wale wale waliokamua vizuri katika THIS IS IT safari hii tuko bush ni full vituko na vunja mbavu,bado nasimama katika msimamo wangu wa kuinua vipaji vya watoto wadogo kabisa nadhani hata ninyi ni shahidi wa hilo,uncle jj,jenifa na patriq twakamua humu chini ya kampuni yangu ya KANUMBA THE GREAT FILM,nikitumia vifaa vyangu mwenyewe nilivyonunua yaani kuanzia camera hadi vifaa vya editing ni vyangu tofauti na mwanzo ambapo ilikuwa ikinilazimu kukodi,hakika najivunia hili kwani kwa sasa nafanya kazi bila presha na namshukuru Mungu kwa hatua hii kuanzia kuwa na kampuni yangu mwenyewe,ofisi yangu lakini kubwa zaidi ni kumiliki vifaa vyangu mwenyewe vya production kuanzia shooting hadi editing Uncle jj na Jenifa ktk makamuzi

Tukishangaa kitu katika scene

Patriq na Jenifa yaani hapa wanangu wamekamua kisawasawa mpaka nimejivunia kuwa nao,nikajivunia kuwaleta katika ulimwengu wa sanaa ya filamu maana ni moto wa kuotea mbali ni zaidi ya This is it

Kama umetizama This is it lazima utajua moto wa huyu Jenifa sasa hapa kituko alichokifanya me si sisemi mtaona tu jamani ndo napika mambo

Patriq na watoto wenzie

Toka niwatambulishe katika ulimwengu wa filamu Jenifa na Patriq kupitia filamu yangu ya This is it wamekuwa gumzo mtaani hata kwa watoto wenzao kila wanapopita inawalazimu kupiga picha na wenzao jambo ambalo nao kwa sasa wanaanza kuzooea hawakatai maana nimeshawafundisha nini maana ya kuwa Star,mbali na hayo nawasimamia shuleni kuhakikisha wanasoma vizuri na kupata elimu bora hii ni kutokana na uwezo wao katika sanaa

Asilimia kubwa Jenifa ndie anayepata usumbufu mkubwa sana kuliko mwenzie lakini bado anaonesha upendo kwa watoto wenzake na kuwajali kama hivi unavyoona

Jenifa kazini mbele ya camera

The great na Cameraman wangu Farid Uwezo ambae ndio mara ya kwanza nafanya nae kazi,kila mara anasema kwa mda mrefu sana nilitamani kufanya kazi na wewe na leo ndoto yangu imetimia tena nikitumia camera yako ya kiwango cha juu,Jamani hiyo ndio camera yangu ninayomiliki kwa sasa chini ya kampuni yangu ni kifaa ninachojivunia kukinunua maana uwezo wake ni mkubwa mno katika picha pia ni producer wachache sana nchini wanaotumia na kumiliki camera kama hii,ni SONY DSR 390

Sep 4, 2010

SAKATA LA SIMU KUUA LAMTATIZA THE GREAT

Toka jana kumekuwa na msg ambazo tunatumiwa katika simu ambazo kwangu zimekuwa nyingi sana zikisema..''Ukipigiwa simu kwa private number au ikiandikiwa call kwa red colour usipokee ni mionzi unaparalise na kufa.Imetokea Kenya na watu wamekufa.Julisha ndugu na jamaa wote''Sasa asubuhi ya leo nikawa napata simu nyingi zikiandika call ila kwa maandishi meusi kitu ambacho nimekizoea maana mara kwa mara hupokea simu za namna hii toka nje lakini kutokana na msg hizi zilizokuwa zikitumwa nikajikuta sipokei toka asubuhi mpaka majira ya jioni baada ya kusoma gazeti fulani lililosema kuwa ''TCRA YAKANUSHA UVUMI ULIOENEA KUWA SIMU KUUA''Ndipo nikaamua kupokea simu hizo ambazo toka asubuhi zilikuwa zikipigwa kwa wingi maskini hata nilipopokea simu niliiweka mbali na sikio na kuweka loud speaker cha kushangaza kumbe ilikuwa simu ya kazi toka India nikaumia sana maana walinilalamikia kuwa toka asubuhi walikuwa wananipigia sipokei.AMA KWELI SAKATA HILI LA SIMU KUUA LIMENITATIZA.

THE GREAT NDANI YA UBALOZI WA NIGERIA

The great nimepata mwaliko toka ubalozi NIGERIA kwa mazungumzo fulani ambayo soon ntawajulisha yanahusu nini,moja ya sababu zilizoangaliwa ni jinsi ninavyoshirikiana na wasanii mbalimbali toka NOLLYWOOD-NIGERIA vizuri hivyo ubalozi ukaona ni vyema uwe na mazungumzo kidogo na mimi. Chiff,the great na minister Ofon Etuknwa katika ofisi yake hapo ubalozini



Nlipatia minister zawadi ya movie zangu baadhi nilizowai kushirikiana na Nollywood stars,nae alifurai sana

THE GREAT ATEMBELEA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO

The great niliamua kutembelea kijiji cha makumbusho kuona asili yetu kama kawaida huwa nasema napenda sana ADVENTURE The great nikikizunguka kijiji

Kwa raha zangu

The great huyooo

Nikamaliza ziara yangu kwa kutizama ngoma za asili

Kwa umakini nikitazama,nikikumbuka enzi zile kaole sanaa group tulikuwa tukicheza ngoma hizi

Hakika nimepata burudani ya nguvu

THE GREAT ATEMBELEA MADUKA YA VINYAGO MWENGE

Leo nimetembelea maduka ya vitu asili na vinyago maeneo ya mwenge nikiwa natafuta kitu fulani kwa ajili ya shooting ndipo nikakutana na mashabiki wangu nao kwa furaha wakanipa zawadi mbalimbali kunipa pongezi kwa kazi zangu. The great na mama Flora aliyenipa zawadi ya viatu(open shoes)mama huyu anaitwa mama Flora jina la mama yangu mzazi


Ikabidi nami nimuunge mkono kwa kununua picha ya ukutani kama pambo

Gafla alitokea shabiki wangu mwingine aliye upande wa kushoto wa picha na kunipa zawadi ingine kama mnavyoona hakika nawashukuru sana mashabiki wangu Mungu awabariki

Niliitwa katika duka lingine la mama baby au Marietha pichani nae baada ya kumuungisha kwa kununua picha asili nae alinipa zawadi ya hicho kinyago pichani.....Asante sana mama baby endelea kutizama kazi zangu

Nikiwaaga na kuwashukuru mashabiki wangu kwa upendo na uzalendo wa kweli kwangu

Sep 2, 2010

GAME 1ST QUALITY TZ LTD YAJA NA DON'T CRY 4ME.

Rose Ndauka kazini katika movie hii


Hemed a.k.a Jembe akiwa kazini

Shooting ikiendelea



Production manager Maya

Aunty na Bi Tumaini nao wamo humu ktk movie hii kali

kazi ikiendelea

Rose akidakwa na Lusubiro mara baada ya kuanguka ili asiumie


Umati wa watu wakishuhudia kazi inavyokwenda

Gwantwa akisubiria action aanze