Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Dec 23, 2010

KWA WALE WAPENZI WA VUVUZELA ZAWADI YA X-MAS HIYOOO

TANGAZO..

Dec 22, 2010

BAADA YA KUMALIZIKA KWA KISHINDO SHOW YETU YA MWISHO BUKAVU MBUNGE WA BUKAVU ALITUKARIBISHA KWA CHAKULA NA VINYWAJI HOTELINI KWAKE MIMI NA SWAHIBA.

Honorable DAVID OMBENI Mbunge wa Bukavu akiwa mjini Kinshasa katika kikao chao cha mwisho cha bunge la DRC alipata habari kuwa katika jimbo lake vijana tumefika hivyo basi kutokana na kwamba alishindwa kuhudhuria show zetu zote za Bukavu jioni yake alipanda ndege na kutualika mimi na swahiba katika Hotel yake ya kifahari ijulikanayo LE V.I.P HOTEL kwa ajili ya chakula cha jioni. Kutoka kushoto wa kwanza ni dereva aliyetumwa kutufata,wa pili nae ni mbunge,Swahiba,The great,Honorable David Ombeni na Socrates.

Mheshimiwa David,Swahiba,Sonia(mtoto wa mheshimiwa mmoja Congo)The great na mheshimiwa mbunge.

SHOW YETU YA PILI BUKAVU

Show yetu ya pili mjini Bukavu ilifanyika uwanjani ambapo umati ulikuwa ni mwingi sana kitu ambacho kilipelekea watu wawili kufariki,na wengine saba kulazwa hospitali kama majeruhi.Mungu alaze pema roho za mashabiki wetu waliopoteza maisha yao(Bukavu) maana lengo lao lilikuwa jema kutuona sisi,Na walioko Hospitali twawaombea uzima na afya tele zaidi ya yote twawapenda sana,lakini twashukuru kwa upendo wa dhati mliotuonesha,MUNGU IBARIKI BUKAVU. Irene Uwoya akiingia uwanjani huku akilindwa na askari polisi na wanajeshi.Huku anajulikana sana kama Oprah.

Tukiwa stejini tukiwapa raha mashabiki wetu

Hii ni sehemu mojawapo ya umati wa watu uliofurika uwanjani

Upande mwingine.

SAFARI YETU KUELEKEA OFISINI KWA WAZIRI WA UTAMADUNI BUKAVU.

Tukiwa Bukavu tulipata mwaliko kumtembelea waziri wa utamaduni Bukavu,hivyo msafara mzima ulikuwa hivi. Baadhi ya mashabiki waliokuwa wakituona waliyazonga magari tuliyomo hivyo kusababisha foleni kubwa barabarani kama unavyoona.

Safari ikawa ngumu kidogo maana mashabiki walitaka kutuona na tuwasalimu kidogo nasi ikabidi tufanye hivyo kama unavyoona Jeniffa akiwa juu ya Gari kuwaridhisha mashabiki.Kwa upande mwingine Jenifa amekuwa kivutio kikubwa sana kwa watu na amejizolea mashabiki wengi sana Congo.

Tukiingia ofisini kwa Waziri

Nami nikiingia

Aunty akipokelewa mlangoni

Tukibadilishana mawili matatu na mheshimiwa mbele yetu aliyekaa mwenye suti nyeusi

Mheshimiwa aliomba tusaini katika kitabu chake cha wageni maalumu waliowahi kumtembelea ofisini kwake nasi tukafanya hivyo.

Sehemu ya ujumbe wangu niliokuwa nikiandika baada ya kusaini

Zamu ya swahiba kusaini

zamu ya Irene Uwoya

Johari nae alifata

Aunty Ezeckiel akafata

Mwisho alimalizia Jeniffa.

Picha ya pamoja na mheshimiwa baada ya maongezi na kusaini

Nje ya ofisi ya mheshimiwa waziri mashabiki walijaa kwa wingi wakitusubiri kwa hamu tutoke ili watuone tena.

SHOW YETU YA KWANZA BUKAVU-DRC

The great nikisikiliza maelezo jukwaani kabla ya kupanda,pembeni ni mwenyeji wetu.

Jeniffa nae akiteta jambo na mwenyeji wetu

Aunty na Johari wakipiga kinywaji aina ya Primus(pelisa ngwasuma)kabla ya kupanda jukwaani

Me na Swahiba tukitambulishwa jukwaani.

Show ikaanza,tulifungua kwa sebene la kufa mtu mimi na Swahiba ukumbi ukalipuka kisawasawa

Aunty,Johari na Jeniffa wakiwa tayari stejini

The great nikiendelea kukamua

Mmoja wa ma bosi wa kampuni ya Steps entertainment Jairad tuliyeenda nae akipose kwa picha na Jennifa

OFF SIDE KUINGIA MTAANI KESHO KUTWA TAREHE 24.

Wakati Congo wakiwa tayari wameshaanza kuiona filamu hii niliyocheza na swahiba wangu hapa kwetu bongo itakuwa mtaani tarehe 24 yaani kesho kutwa ili mashabiki wetu wakila x-mass huku wakitazama OFF SIDE..Hakikisha unanunua nakala yako ORIGINAL na SIO FEKI au KUMUAZIMA JIRANI YAKO,NI VYEMA UKAWA NA NAKALA YAKO,TUWE WAZALENDO KWA KUPENDA KAZI ZANYUMBANI.
Poster la movie Off Side linaonekana hivi......nikiwemo mimi,Swahiba,Irene Uwoya,Jb nk.

Dec 20, 2010

ZIARA YETU NCHINI CONGO katika uzinduzi wa filamu yetu ya OFF SIDE.

Jumatano iliyopita saa sita za mchana,The great,swahiba,Jenifa,Johari,Aunty na uongozi wa STEPS tulielekea nchini Congo kupitia KIGALI-RWANDA katika kuzindua movie ya OFF SIDE,Blog hii inakuletea matukio ya safari nzima na jinsi ilivyovunja rekodi kwa umati wa watu na mapokezi ya nguvu,mpaka sasa bado tuko huku Congo na hali imekuwa ni ya kushangaza. Tukiwa uwanja wa MWL JK Nyerere tukisubiri kuondoka

Ndani ya ndege Johari,Jennifa,na Aunty katika pipa kwenda Congo kupitia Kigali

Pritesh kushoto na Jairad kutoka Steps

Me na Swahiba pipani

Jennifa alianza kutapika wakati ndege ilipoanza kushuka

Tukiwasili uwanja wa ndege wa Kigali na mapokezi yakawa hivi

Katika basi tukitoka airport sasa Jennifa yuko fiti hatapiki tena

Mashabiki walifunga mitaa na barabara kwa kutupokea kwa shangwe

Umati umetuzunguka na kutufata popote tuendapo

Umati mkubwa wa watu,barabara na mitaa imefungwa huku ulinzi wa polisi ukiongezwa kila mara kutokana na watu kujaa sana barabarani na kusababisha foleni kubwa sana ya magari

Nikihojiwa na waandishi wa habari toka magazeti,radio na tv mbalimbali za Rwanda

Umati mkubwa sana wa watu(mashabiki)wakitushangilia...NITAENDELEA KUWAJULISHA YANAYOJILI HUKU HIVYO TEMBELEA BLOG HII KILA WAKATI MAANA NI BALAA

PICHA ZAIDI KATIKA FUNGA MWAKA PARTY YA STEPS ENTERTAINMENT CO.LTD

Jacklyn wolper na Odama katika mnuso

Bwana harusi na mkewe (Chiki)walikuepo

Danny Basila kushoto mkurugenzi wa kampuni ya Christian promoters alikuepo

Jimmy master,Chuzz,na Raisi wa wasanii Mwakifwamba walitoa shukrani zao kwa niaba ya wasanii wa filamu

Steps family

Boss wa Steps DILESH SOLANK akitoa hotuba fupi kuhusu kampuni yake na malengo yake kwa wasanii wa filamu kwa mwaka 2011.

Burudani toka THT

Wasanii na wadau walijimwaga uwanjani kucheza mziki

The big two na Mwanajeshi tukipata picha

Story za hapa na pale.