Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jul 30, 2011

UMEME UWAKE USIWAKE ''DEVIL KINGDOM'' LAZIMA ISONGE MBELE

KUTOKANA NA TATIZO SUGU LA UMEME TULILONALO HAPA BONGO,NA KUTOKANA KWAMBA SITAKI KUWAANGUSHA MASHABIKI WANGU JUU YA UJIO WA FILAMU YANGU MPYA YA DEVIL KINGDOM NIMEAMUA KUNUNUA GENERATOR YENYE UWEZO MKUBWA WA KUWASHA TAA,AIR CONDITION,COMPUTOR NA VIFAA VYOTE VYA OFISINI VINAVYOHUSIKA KATIKA KUHARIRI MOVIE ILI SHUGHULI YA EDITING IENDE KAMA NILIVYOPANGA MSICHELEWE KUIONA MOVIE,TANESCO WAKICHUKUA UMEME WAO NAMIMI NAWASHA WANGU KAZI INASONGA MBELE OFISINI ...WAHENGA WANASEMA SHIDA DARASA..... GENERATOR YANGU IKIFANYA KAZI YAKE MAANA UMEME NDIO HIVYO TENA.


HAKIKA INA UWEZO MKUBWA HADI KUSUKUMA AIR CONDITION MBILI.


OFISINI KWANGU ZAKAYO MAGULU AKI-EDIT DEVIL KINGDOM


TUKIWA SAMBAMBA KATIKA KUHARIRI ILI KITOKE KITU KIZURI


TUKIWA MAKINI NA KAZI,UMEME WA HAPO SI TANESCO BALI GENERATOR BILA HIVYO HUTOFANYA KAZI MAANA KUNA SIKU UNAKATWA KWA SIKU MBILI BILA HATA KUWASHWA KIDOGO.

Jul 25, 2011

''DEVIL KINGDOM''prince of the world........tuonane mwezi wa nane sokoni...

Patrick nae yumo


Patrick kazini











SWEBE nae yumo ndani ya movie hii......sokoni mwezi wa nane jamani.....

SCENE ZA MWISHO MWISHO KATIKA DEVIL KINGDOM...

Hii ni movie inayoingia katika historia yangu ya movie niliyowaikushoot kwa mda mrefu kuliko zote nilizowaikushoot,ni movie iliyoshirikisha washiriki wengi main na extras kuliko movie yoyote niliyowaikushoot au zilizowaikutengenezwa hapa bongo maana ni zaidi ya washiriki mia mbili,ni movie iliyoitaji vifaa vya ziada katika shooting,lakini hata mfuko kidogo dah umetumika...sokoni mwezi ujao....DEVIL KINGDOM scene za kanisani


kwaya





kazi ikiendelea


washiriki katika scene








Toba ya kweli








The great kazini


Scene kama hizi huwa sifanyi makosa huwa nazitendea haki kikweli na huwa najiandaa,


Huwa nahakikisha hata kama kulikuwa na mtu anapiga kelele basi huwa aambiwi nyamaza bali hunyamaza mwenyewe kwa kutizama,Scene ngumu kama hizi ndipo uonekana uigizaji wa msanii na kiwango chake katika Acting.


Hii scene hata ujifanye eti ooh sitazamagi movie za kibongo....utatizama tu hata kwa siri chumbani kwako,mdomoni utakataa ila rohoni utakubali maana ndio asili yetu,....Sokoni mwezi ujaoooooo

Jul 21, 2011

NAOMBA TUCHANGIE WADAU JE? POMBE NI DHAMBI?

Niliamua kumtembelea rafiki yangu baba PAROKO Maganga wa kanisa la SINZA kufafanuliwa kuhusu pombe,niliamua kufanya hivyo kutokana kuwa na kauli tofauti toka kwa watu kuhusu pombe,wapo wanaosema pombe ni dhambi,wapo wanaosema unywaji wa pombe kupindukia ni dhambi,wapo waosema pombe ni haramu,lakini yapo madhehebu ya dini ambayo yanaruhusu unywaji wa pombe na yapo yanayokemea kabisa hata kugusa,na wote hao hutoa mistari toka katika Biblia takatifu kama kidhibitisho,Hii haimanishi mimi ni mnywaji wa pombe lakini ebu tujadili hili toka katika maisha yetu ya kila siku,toka katika maandiko ya vitabu vya dini lakini pia toka kwa wanafalsafa mbalimbali duniani na viongozi wetu.Katika utafiti wa kwanza niliofanya toka kwa Paroko yeye alisema....''''Pombe ni kama kisu,ukikichukua kisu kukatia nyanya na vitunguu kisha ukapika chakula watu wakala hapo kisu ni kizuri,....ILA ..ukichukua kisu hicho hicho na kwenda kumchoma mtu na kumjeruhi hapo kisu ni kibaya,hivyo basi hata pombe ukinywa na kwenda kufanya yasiyofaa hapo ni mbaya kwako lakini ukinywa na bila kufanya mabaya hapo si mbaya hivyo inategemea na unavyoitumia yenyewe haina ubaya.'''''Jamani wanywaji na msiowanywaji ebu tuchangie hapa............... Nikiwa ofisini kwake akinielekeza mambo mengi kuhusu Dunia


Mimi huwa napenda sana kudadisi kwa kuuliza maswali hapo nikiuliza swali?


Akinifafanulia jambo kwa umakini zaidi


Ukiwa katika ofisi za watumishi wa Mungu mda wote unajihisi kutakasika...


Baada ya maongezi alinisindikiza na tukapata picha ya pamoja


Hakika nilijifunza mengi sana hivyo nikawa nimeongeza vitu kichwani ila kwa leo tu naomba tujadili kuhusu POMBE...

Jul 18, 2011

ILIVYOKUWA SURPRISE BIRTHDAY YA HARTMAN MBILINYI ALIYOFANYIWA NA MKEWE MARIAM HARTMAN(mama wa London)

Hii ilikuwa nyumbani kwa Shyrose Bhanji-Mbeziiiii.... Alivyoingia tu akamwagiwa kimiminika hicho toka kwa swahiba


Akipongezwa


Mkewe akajitokeza........





Steve Nyerere yeye aliamua kukaa karibu na meza yenye vinywaji ili asipate tabu kuagiza


Hartman,The great pioneer,swahiba


Shyrose,Hartman,Mariam Hartman


The BIG TWO tukiteta...


MR&MRS HARTMAN MBILINYI





Wakati wa kucheza mziki.....

Jul 16, 2011

ZANTEL YAANDAA TAMASHA LA WAZI LA MUZIKI KUPITIA OFA YAKE MPYA YA EPIQ NATION.

Msanii kutoka Kenya Nameless akitumbuiza na madansa wake kwenye jukwaa la EPIQ NATION coco beach jumapili iliyopita.


Chidi Benz akiwarusha mashabiki wake wakati wa tamasha la EPIQ NATION coco beach


Baadhi ya wafanyakazi wa ZANTEL wakila shangwe katika tamasha la EPIQ NATION


Msanii wa kike MWASITI nae alikuepo kuwasha shangwe katika tamasha la EPIQ NATION coco beach hapo


Palikuwa hapatoshi coco beach,EPIQ NATION....JANJARUKA NA KREW MPYA MTAANI

SCENE ZA MWISHO MWISHO ZA DEVIL KINGDOM

The great na bi Mwenda








me na kajala


hii picha niliipenda tu kila mtu alivyo busy


scene


location





kama watoto huwa karibu yangu location


shooting