Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jan 24, 2012

BEST ACTOR ZIFF AWARDS (2011/2012) NI STEVEN KANUMBA.,NA BEST FILM IN SOUND NI MOVIE YANGU DEVIL KINGDOM.

Nikipokea tuzo yangu ya Best actor kutoka kwa Mr.Danny wa ZIFF,Shukrani zangu za dhati kwa majaji,shukrani kwa waandaaji,shukrani kwa mashabiki wangu wa roho na kweli,shukrani kwa walionipigia kura na kunipendekeza,zaidi ya yote sifa na utukufu nitaendelea kumrudishia mfalme wa maisha yangu YESU KRISTO na MUNGU BABA maana yeye ndiye aliyeniahidi ktk Biblia yake takatifu kuwa nikimtumaini yeye atanifanya kuwa kinara na si mkia tena atanifananisha na mlima Sayuni sitoteteleka milele,waigizaji wazuri tupo wengi ila imempendeza Mungu nichukue mimi tuzo hii kuwasilisha uzuri wa wengi tulionao.
Kaka yangu JB alichukua tuzo ya filamu bora(Senior bachelor)hongera sana kaka yangu nakumbuka baada ya kutizama filamu hii nilikupigia simu kukupongeza hasa kwa stori na uchezaji wako,mwandishi Vincent Van Goh anasema...appreciate people so that one day u ll be appreciated,if u don,t do that no one will appreciate you,,
Hiyo ilikuwa ni tuzo ya msanii bora chipukizi.....
Kambarage akipokea tuzo ya Steps Entertainment co Ltd kama kampuni bora ya usambazaji wa movie.
The great nikipokea tuzo ingine ya BEST FILM IN SOUND(DEVIL KINGDOM)hii ni ile niliyocheza na swahiba Ramsey toka Nigeria,Filamu zenye ubora huu wa sauti zipo nyingi ila imempendeza Mungu Filamu yangu kuchukua tuzo hii kuwakilisha ubora wa sauti katika filamu zetu tulizonazo.
Issa Musa(Cloud)akichukua tuzo ya BEST DIRECTOR,Hongera sana kaka yangu kumbuka Chanda chema siku zote huvikwa pete.
Picha ya pamoja ya washindi wote wa tuzo waliokuepo jana maisha club......
Interview ya Cloud mara baada ya tuzo nae kama kawa alilia na bodi ya filamu.....
Kwa niaba ya Ray ambaye hakuepo ukumbini nilimchukulia tuzo yake ya THE MOST INFLUENTIAL ICON.




Maneno yangu ya mwisho mara baada ya tuzo yalikuwa ''Hata tukiwa na uwezo wa kuhamisha milima kama hatupendani ktk tasnia ni kazi bure,kile kilicho moyoni ndio kioneshe usoni na sivinginevyo kama wanichukia moyoni basi onesha usoni na kama wanipenda moyoni basi onesha usoni na si vinginevyo,Isiwe moyoni wanichukia alafu usoni wanichekea,Hii sanaa ni karama tuliyobarikiwa na Mungu tuitumie vyema kwa ajili ya utukufu wake maana ipo siku atatuuliza na kutudai,kama katupa bure basi anao uwezo wa kutuny'ang'anya pia''soma Wakorintho uone jinsi Mungu alivyogawa karama hizi na ni kwanini katugawia.,

Jan 23, 2012

ZIFF AWARDS NA RED CARPET YAKE ILIVYOFANA MAISHA CLUB.....

The great mara tu baada ya kuingia club Maisha na kupita red carpet interview mbalimbali zilianza kama unavyoona hapo.Hongera sana waandaaji wa tuzo hizi ZIFF.Hongera Mr,Danny.Kauli mbiu ya tuzo hizi na red carpet ilikuwa kuhimiza jamii kununua kazi ORIGINAL za movie hapa nyumbani na si FEKI,lakini pia kuhimiza uzalendo wa dhati kabisa katika sanaa ya nyumbani hususani filamu,
Odama na Maya nao walikuepo hapa maisha club.
Movie stars mbalimbali waliitumia siku hii kama siku yetu maalumu.
JB akihojiwa hapo ktk red carpet.,Pia akilia sana na bodi ya filamu juu ya mambo wanayotaka yafanyike ktk tasnia.
Irene Uwoya,msanii na Mzee Magali walikuepo
Richie Richie,Monalisa na Mama Natasha walikuepo.....
Hapo nikitoa maoni yangu juu ya sheria mpya zilizotolewa na Bodi ya filamu nchini ambapo karibia wasanii wote nchini wamezipinga na kuzikataa maana zinaua tasnia hii ambayo tumepata shida sana kuifikisha hapa ilipo,Leo watu wachache tu bila kufanya uchunguzi wa kina wanaweka vitu ambavyo ni ndoto kwa wasanii sie tunaoibiwa kazi zetu na tusio na soko maalumu kuzitimiza
Interview ikiendelea hapo.......
Tino,Dinno,Mzee Chilo,Baby Madaha walikuepo...
Irene Uwoya katika interview lakini pia nae hapo akishangaa hizi sheria za bodi ya filamu,,,,
Pilipili Entertainment nao walikuepo...
Big boss Mr.Dilesh wa Steps entertainment akiteta jambo na Richie Richie...
Edwin Kileo mzee wa Subtitle alitaka kuhakikisha kiatu changu kama kweli ni CL toka Paris-Ufaransa nami nikamhakikishia...ahhahah Wazee wa pamba mnajua hii manenoooo,,,,?????
Furahia Swahili movie na nunua kazi original na si feki na kuwa mzalendo wa kazi za nyumbani kumbuka mcheza kwao hutunzwa na mkataa kwao mtumwa.

Jan 22, 2012

THE GREAT NDANI YA MKASI WA SALAMA JABIR

Baada ya kuwa busy sana toka mwaka jana hatimae nikapata mda wa kurekodi kipindi cha mtangazaji wa EATV na rafiki yangu dada Salama Jabir.....picha hapo juu nikiingia ktk hiyo salon tayari kwa kuanza...
Picha kidogo za pamoja zinazoonesha upendo na umoja,kushoto ni Dida,Me na Salama.
The great nikiingia....
Huku nikisafishwa kucha huku mahojiano yakiendelea ambapo nilitoa ushirikiano wa dhati.
Le presedar Nyoshi El Sadaat sauti ya simba nae alikuepo kutoka FM ACADEMIA.
Hapo akiniambia kuwa nayeye anataka kucheza movie ya kihistoria nchini.
Swahiba na mzee wa njaa mwenzangu A.Y nae alikuepo
Kwa pamoja tukafanikisha kipindi cha MKASI ambacho kitarushwa soon kaeni mkao wa kutizama maana nina mda sana sijafanya interview kama hizi.

Jan 20, 2012

NANI ZAIDI KATI YA JENNIFER NA SOPHIA?JE UNATAKA WAKUTANE KTK KAZI MOJA?

WAWEZA TOA MAONI KWA HAWA WATOTO WAWILI SOPHIA AMBAYE NDIYE ANATAMBA SANA KTK MOVIE YA BIG DADDY NA JENNIFER KTK THIS IS IT NA UNCLE JJ,NANI UNADHANI NI ZAIDI YA MWENZAKE???(hakikisha umetazama movie zao zote yaani big daddy na uncle jj au this is it ndio utoe maoni yako)JE UTATAKA WAKUTANE KTK KAZI MOJA AU KILA MTOTO AENDELEE NA MOVIE KIVYAKE????karibuni....
SOPHIA KATIKA POZI a.k.a why..why...why????
SOPHIA akiwa na BIG DADDY/UNCLE JJ.
JENNIFER ktk pozi......
MOJA YA KAZI ALIZOFANYA JENNIFER ILIYOMPANDISHA.

PICHA YA WEEK.........

THE GREAT&MADAM RITA.

Jan 17, 2012

KWA WALE WALIOHITAJI KUJUA GHANA NILIENDA KUFANYA NINI NA NITAFANYA NINI,JIBU NDIO HILI....




Bleeding Sunshine: A Hollywood Thriller on Human Trafficking

Female film makers from Africa have taken the continent’s movie industry a step further in recent times. Female directors, Chineze Anyaene in Nollywoods most successful film ,Ije and Leila Djansi’s-Sinking Sands from Ghana are few classic examples. We about to witness another landmark achievementes an US-based Ghanaian filmmaker, Yaa Boaa Aning, parts the curtains for Bleeding Sunshine; an international feature film on human trafficking.

Yaa has just wrapped up the Ghana shoot of the feature but would take shots from some other significant locations in Egypt, Dubai and Israel.
Bleeding Sunshine sheds light on the intricacies of human trafficking with emphasis on African teenagers trafficked to other parts of the world especially to Europe for commercial sexual exploitation.It tackles some of the modus operandi of traffickers while sharing information on victim’s ordeal.

This brings to bare the nightmares of a young Ghanaian girl played by Suzzy Norbile who was adopted from her humble fishing village and thrust into the gritty world of international human trafficking.

Yaa Boaa Aning wrote the film’s script five years ago when she was doing a research on Interpol. Through the research, she came across an article, which inspired her to further investigate human trafficking cases.

Yaa Boaa, a University of North Carolina Alumni, has worked in Hollywood for the last decade, is fascinated by the beautiful locations in Ghana and said it was one of the factors that inspired the feature.

“I mean it is so beautiful out here. Part of the reasons to shoot was to show Ghana in a way, it has never been shown before to the world before. There is going to be photo-tourism. Everywhere we turned our camera there is richness of culture and we want people in abroad to see and remind people that leave here how special this place is and also inspire them to look after it,” she told Daily Guide.

“There were certainly some challenges. But the benefit is just how great the locations are here. We shot in Prampram in an abandoned Polo Club with the view of ocean & horses running in the background. We also did a number of sunrise shots with fishermen pushing their boats out into the ocean and the sun coming up behind them. There are incredible scenes out there that I don’t get to see in Hollywood. You know it is something so different. It is really great. The pictures have never been done before,” added Chase Bowman, Director of photography (DOP) of Bleeding Sunshine.

Chase is a top Hollywood DOP with feature film credits like the Warner Bros. release “Listen To Your Heart” featuring Cybil Shepherd; “In a Pickle” starring Jackie Mason, and “Cost of a Soul”, which was theatrically released nationwide at 50 AMC theaters in April 2011.

He started shooting professionally at the age of fourteen, refined his skills by studying art and photography in Rome, and ran his own production company for ten years.His involvement in Bleeding Sunshine is his first experience working in Ghana and second in Africa (Kenya was his first).

With heart-throbbing scenes, the story Bleeding Sunshine is told with a great cast from around world; one reason the movie is expected sells internationally aside its theme.

Although, Hollywood cast are to be made public, the film’s African cast will include Hotel Rwanda star Hakeem Kae-Kazim, “2011(AMAA) Best Actress - Ama K.”2011 Pan African best Actor- Chris Attoh, 2010 (AMAA) Best Actor–Adjetey Anang (Pusher), 1996 Oakland Black Film Achievement Winner - Amonobea Dodoo, 2011 Tanzania”s Best Actor -Steven Kanumba, 1998 USIS Award Winner-Omar Sheriff Captan, Amonobea Dodoo–1996 OakLand Black Film Achievement Winner with new-comer Suzzy Norbile, , Jasmine Baroudi, Lady Arafua, Afro-Soul sensation Katou whose single” Happy Endings” just set the R&B charts on fire & Lucy Kwao with other African casts.

“I played the character of Captain Addo, a fisherman, the father of Suzzy, the girl who was trafficked overseas.It is great production and very professional. I was always on my toes because I knew that I have to raise my level. It wasn’t a layback experience or like what we have back home. The director and crew were down to earth,” Adjetey Anang said about his role in the project.

Yaa Boaa began her career in advertising in NY. But boredom with the lack of creative expression, she decided to try her hand at fashion show production with some of the most famous houses in the world–Giorgio Armani, BCBG and Betsey Johnson etc.

Fashion Styling production lead her to film costuming, which ultimately exposed her to film making, working with such acclaimed directors as Michael Mann, Bill Condon and John Singleton. Never letting go of her passion for writing, between 2007 & 2010, Yaa Boaa completed her first 5 film scripts.

In 2009 she wrote and directed award winning short, The Prince of Venice. Other projects include Felix Triangle for President, which is currently in pre-production and Zahara in post-production.


Yaa is
known for production roles in Hollywood movies and television series such asFast & Furious, ‘The Goods Live Hard, Sell Hard’, ‘xXx: State of the Union’, ‘Just Legal’, ‘Flight of the Phoenix’, ‘Out of Time’ and Private Practice.She costumed Jamie Foxx and Usher in ‘The Kingdom’, ‘Dream Girls’& ‘Miami Vice’’.

Richard Nwaobi-E project manager for the film says, “it’s been great working with such a talented and diverse African cast and crew on this film”. He assembled the great cast as the film producer, along with Dave Boapomg theproduction manager, Corey Geigner - Assistant Cameraman with Brian Angels.

Jan 14, 2012

NITAKUKUMBUKA DAIMA MZEE KIPARA.

Ni wazi Mzee wetu Mzee Kipara hatunae tena,na hapa ndipo tunapouona ukuu na uwezo wa Mungu ushindao akili za mwanadamu maaana kama wanadamu tungelikuwa na uwezo wa kuzuia KIFO basi tungezuia ili tubaki na Mzee wetu,Kwangu mimi binafsi nitamkumbuka sana Mzee huyu hasa kwa mambo yafuatayo;
1.Kwangu alikuwa kama baba mzazi tena mtoto wa pekee,alinipenda sana nami nilimpenda hii utaiona hata pale alipoumwa nami nikawa nje ya nchi aliuliza mara kwa mara Kanumba hajarudi?Lakini pia kati ya namba za simu alizokuwa amezishika kichwani za wasanii wote wa Kaole nadhani ya kwangu ilikuwa mojawapo hakuitaji kuisave.
2.Mzee Kipara ndiye aliyenipokea wakati najiunga Kaole mwaka 2001 na kuhakikisha napata nafasi ya kuwa kundini humo na kufanyiwa interview,kipindi hiki alinisisitiza sana kuwahi na kufanya mazoezi,alinisihi kuacha mzaha na kujibidiisha kundini humo maana Sanaa alijua itanifikisha mbali.
3.Alinisisitizia sana Shule na kunitetea hasa pale nilipochelewa mazoezini Kaole kwa sababu ya kuchelewa kutoka shuleni nikiwa secondary,wapo viongozi ambao waliniambia soma kwanza sanaa baadae ila yeye alinitengea mda maalumu mbali na ule wa saa nane bali nilifika saa kumi au tisa na kufanya mazoezi ,Hapa alisisitiza kuwa Sanaa yahitaji Elimu hivyo soma mwanangu.
4.Alipenda sana Ukimya na Upole wangu na hapa aliongea kwa ukari kwamba Usijifanye mpole hapa ukishakuwa staa uanze kuwa kimbelembele,kwa hili nimeendelea kumthibitishia hadi pale mauti yalipomfika hakuwai kuona tofauti yangu kitabia tangu niko Kaole sijulikani hadi nilipojulikana.
5.Alinisihi sana kujiepusha na Ugomvi wowote ule,bali hekima na maarifa walinijaza yeye na marehemu Mzee Pwagu,kuna wakati walinitania wakisema weeee Kanumba ebu tizama mimi na mzee mwenzagu Pwagu tangu ujana wetu hadi sasa hatujawai hata kunyoosheana vidole,vipi nyie vijana mpigane ngumi na kurushiana maneno?siku nikikuona unapigana nakutandika na hii bakora yangu...hapa wote tulichekaa,Jambo hili nililimudu tangu Kaole sikuwai kupigana na mtu yoyote iwe kwa ngumi au kutukanana,Wazee wetu hapa walifanikiwa kutuunganisha kama ndugu walio katika kundi moja kwa upendo,Tizama leo hii hawapo TUNATENGANA,TUNAGOMBANA,HATUPENDANI,CHUKI ZA WAZI WAZI,TUNAJIKWEZA NA KUJIINUA HATA PASIPOSTAHILI,Hapa Mwenyezi Mungu atusaidie sana.Nitamkumbuka kwa utani wake alipopenda sana kunitania nami nilimtania pia,nilichukua fimbo yake na kuificha wakati akitafuta anagundua nimeficha basi anafoka kidogo ila lengo linabaki palepale UPENDO.Alinibariki na kunipongeza kwa kila hatua nzuri ya kisanaa niliyopiga,Alinitia moyo pale nilipojikwaa,Alinifariji pale nilipoumia,na akafanyika rafiki wa kweli.Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi..amen.
Hapa ni siku niliyomtembelea kigamboni wakati alipoanza kusumbuliwa na matatizo ya miguu mwaka jana.
Nilimpatia kiasi kadhaa cha fedha kwa ajili ya kupata mahitaji mbalimbali hapo alipokuwa.
Ni kawaida yake alipenda kushukuru,kubariki na kukuombea dua.
Pamoja na kwamba miguu ilikuwa inamsumbua lakini alijitaidi kunisindikiza.
Hapo ni stori mbali mbali za hapa na pale..nikiiba hekima na busara za wazee.
Hapa alivyokuwa akinielezea miguu inavyomuuma na jinsi tatizo lilivyoanza.