Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Feb 22, 2012

EBU PATA PICHA.......

JENIFER NA SOFIA


PATA PICHAAAAA
AHAHHAHAH GUSA GUSA SOUND....
SOFIA NA PATRICK KTK VOCAL.....
JAMILA KTK GALATON GITAA.
PATA PICHAAAAAA NI NINI HIKI??
JENIFER NA SOFIA...
JENIFER...
KAMA JENIFER AKIPIGA KINANDA UNADHANI SOFIA ATAIMBA???AHAHHAHA PATA PICHA....
AHAHAH ....THE KANUMBA"S,,,,,,
JENIFER KTK KINANDA.......

Feb 14, 2012

EMMANUEL MYAMBA AMTEMBEZA THE GREAT OFISINI KWAKE(BORN AGAIN FILM)

Kwakuwa naujua vizuri mwanzo wa sanaa yake rafiki yangu Pastor Myamba akaona ni vyema pia kama nitatembelea ofisini kwake kuona maendelea yake,nami hakika nilimpa pongezi za dhati kabisa maana mbali na kuanzisha chuo lakini pia ana kampuni yake ila kikubwa zaidi sasa amekuwa msambazaji wa kazi za filamu,hivyo akishoot movie zake anasambaza mwenyewe na ana mashine za kufyatua dvd original si feki hapa.
Akinionesha mashine zake za dvd....
Tukiwa ofisini kwa mkurugenzi Myamba,mie na kijana Nteze.
OFISINI
Hongera sana ndugu yangu...
mitambo mitambo...
Katulia ofisini kwake kijana....
Hapa ni sehemu ya mapokezi,Myamba,The great na Makubi....
Akishuka katika gari yake tayari kwa kuingia ofisini kwake,hiyo ni ofisi yake kwa nje inavoonekana.
Hili ni duka lake la kuuza kanda za filamu mbalimbali...
Dukani karibuniiiiii.............

Nikiweka sahihi katika kitabu cha wageni.

EMMANUEL MYAMBA AZINDUA RASMI CHUO CHAKE CHA FILAMU(TANZANIA FILM TRAINING CENTER,,TFTC)

The great mara baada ya kufika maeneo ya chuo hicho ubungo,nikihojiwa na waandishi juu ya chuo hicho cha rafiki yangu Emmanuel Myamba a.k.a pastor myamba,alichokianzisha kwa lengo la kutoa mafunzo kwa watu mbalimbali wanaotaka kuingia katika filamu.Kwa ufupi Myamba ni rafiki yangu tangu tunasoma wote form five na six Jitegemee high school kipindi hicho mimi tayari nilikuwa naigiza kitambo hivyo mara baada ya kumaliza shule nilimtambulisha rasmi katika sanaa hii ya filamu na nikampa staili yake ya UCHUNGAJI,ambayo iliwavutia wengi mpaka leo wengi hujua ni mchungaji wa ukweli,wakati anaanza anza alikata tamaa kidogo lakini nilimsihi unapoona unakata tamaa jua mafanikio yako mlangoni,nikamsihi asonge mbele tizama leo sasa anaamini maneno yangu ambayo Mungu kamsimamia kutokana na yeye aliwezeshwa katika filamu basi nae kafungua chuo kwa ajili ya kuwasaidia elimu wengine,chuo hicho kinaitwa ''TANZANIA FILM TRAINING CENTER''lakini pia leo hii ana kampuni yake iitwayo ''BORN AGAIN FILM COMPANY''inayotengeneza filamu na kusambaza..Hongera sana Myamba Mungu azidi kukusimamia.
Nikisisitiza kuwa kama sisi tulivyoanzia ktk vikundi kujifunza basi na wasanii wengine waje hapa kupata elimu juu ya uigizaji na si kuingia tu ktk film industry wakati hujui lolote.
Waalikwa tukiwa ndani sasa...
Meza kuu,kutoka kushoto ni Baucha,Myamba,mwakilishi wa katibu mkuu Basata,na Makubi ambaye ni mratibu wa chuo hicho.
Ukisomwa ujumbe maalum wa mgeni rasmi toka Basata.
The great kama mmoja wa walezi na mshauri wa chuo hicho nilipewa nafasi ya kusema machache kwa wanafunzi na tasnia kwa ujumla.
Wanafunzi wakiwa na uniform zao safi kabisa lakini pia humu ndio darasa lao,wanasoma katika air condition,
Bosi wa chuo Pastor Myamba akikabithiwa kibali toka Basata kama ishara ya kwamba anatambulika rasmi na mamlaka husika serikalini.
Wosia toka Basata...msipende kukatishana tamaa na kuharibiana,Basata ipo kwa ajili yenu na ndio walezi na washauri wakuu wenu.
Cheti cha usajili..
Kibali...
Maneno yangu The great kwa wanafunzi yalikuwa;SANAA BILA ELIMU NI SANAA ILIYODUMAA,SANAA YENYE ELIMU NI SANAA ENDELEVU,VIYVO HIVYO KIPAJI PASIPO ELIMU NI GIZA TOTORO,KIPAJI CHENYE ELIMU NI NURU ING'AAYO.NDIO MAANA HATA BIBLIA INASEMA MSHIKENI SANA ELIMU MSIACHE AENDE ZAKE,LAKINI PIA ELIMU PASIPO KIPAJI NI KAZI BURE,BORA USOMEE KITU AMBACHO NI KARAMA YAKO,mfano kama una kipaji cha uchoraji basi somea uchoraji na si uigizaji usijepoteza mda wako bure,ukiviweza vyote hivi basi zingatia nidhamu..wanafunzi walinipigia makofi bila shaka walinielewa.

''KIJIJI CHA TAMBUA HAKI''NI MWEZI HUU JAMANI...

Location.........
Wasanii kazini.....
Kajala na Kanumba kazini.......
Cameraman Zakayo Magulu kazini........
Tukiwa na furaha mara baada ya kumaliza kushoot movie hii
Miziiikii miziikiii......kumaliza movie sio jambo dogo,wapo wengi hushoot na movie huishia njiani.
Kwaitooooooo......
Kwaitoooooo
Kazi ikipamba moto...

Feb 9, 2012

MANENO YANGU KWA MASHABIKI WANGU WOTE WANAOPITIA AU WALIOPITIA MAISHA MAGUMU KTK FAMILIA(,DIFFERENT SEASONS&FLAVOURS) .


THE FOLLOWING PICTURES ARE OF THE SAME BUT TAKEN AT DIFFERENT SEASONS..STAY BLESSED AND ENJOY THE SEASONS OF YOUR LIFE




LESSONS ON LIFE:=U can not judge a tree or a person by only one season,and that the essence of who they are and the pleasure,joy and love that come from that life can only be measured at the end when all the seasons are up.If you give up when its winter u will miss the promise of your spring,the beauty of your summer and the fulfillment of your fall......MORAL:=Don't let the pain of one season destroy the joy of all the rest.Don't judge life by one difficult season.Thank u...Steve Kanumba.