Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jul 3, 2011

MUIGIZAJI WA SEX AND THE CITY KUTOKA HOLLYWOOD(KRISTIN DAVIS) ATUA BONGO KATIKA UZINDUZI WA MAMA SHUJAA WA CHAKULA TOKA OXFAM.

Uzinduzi huu uliofanyika jumamosi asubuhi unampa nafasi mwanamke yoyote nchini aliye mkulima au mfugaji kushiriki katika shindano hili toka OXFAM linaloitwa FEMALE FOOD HERO AWARDS 2011.kuanzia heka 0 na kuendelea unaweza chukua fomu na kushiriki,hii ni njia pekee ya kuwatia moyo mama zetu walio wafugaji na wakulima bila kujali anatumia nyenzo gani.Mimi Steven Kanumba kama balozi wa OXFAM katika kampeni ya OTESHA nikishirikiana na Kristin Davis toka Los Angelos Marekani na Oxfam team tulijumuika katika uzinduzi huu unaohusika nchi nzima na mwakani utakuwa dunia nzima. Kutoka kushoto wa kwanza ndiye KRISTIN DAVIS aliyetua bongo kwa ajili ya kazi hii hapo akiwa katika poster la series yao.


Katika kijiji cha makumbusho ndiko ilifanyika


Mkurugenzi wa OXFAM bi.Monica akifungua rasmi hafla


The great nikisalimia watu kwa kunyoosha mkono


Kristin Davis,kanumba,na mama anayewakilisha akina mama wote nchini wakulima tukiwa meza kuu.


Watu,Taasii,na Makampuni mbalimbali yalikuepo ili kunga mkono kampeni hii inayomsaidia mwanamke,


Dada Mwanahamisi Salim Toka OXFAM akielezea jinsi shindani hili litakavyokuwa na zawadi zake,maana mbali na kupata tuzo mama shujaa wa chakula atapata zawadi nyingine zaidi


Kristin Davis akielezea umuhimu wa mwanamke katika jamii na kuwaita WANAWAKE NI HERO.kabla ya hapa alitembelea morogoro kuona kilimo bora toka kwa akina mama.


Akizindua rasmi shindano hili


Mfano wa tuzo atakayopewa mama shujaa wa chakula


Balozi nikielezea machache kuhusu zoezi hili na haya ndiyo yalikuwa maneno yangu...''Mama zetu wamekuwa wakulima kwa mda mrefu katika hali ngumu bila kukata tamaa lakini mchango wao umekuwa hauonekani wala kuthaminiwa katika jamii ndio maana mimi Steven Kanumba nahamasisha wanawake wote wakulima na wafugaji nchini na akina baba kuwahimiza wake zao kushiriki katika FEMALE FOOD HERO AWARDS 2011(MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2011) ili kuamsha kilimo nchini na kuwatia moyo mama zetu katika sekta hiyo kwa mchango wao mkubwa.


Kristin Davis na The great tukiteta jambo


Nilimuuliza ka swali kadogo katika SEX AND THE CITY alivyonijibu ilibidi nicheke tu maana ni mchangamfu mda wote.


Tukiendelea na ratiba ya hafla


Tukiteta jambo kidogo


mmmmmmmmh????????????'''''

10 comments:

Anonymous said...

KAKA UJE UZAE NA MZUNGU YAANI UOE MZUNGU MTOTO ATOTOKA VZURI ILE MBAYA WEWE UNAONAJE KAKA.

Anonymous said...

Kaka naona jinsi mlivyo pendeza yaani kama wifi vile wai kaka tutauza mbuzi wa tajiri ili kukamilisha mahari.

Anonymous said...

Kaka naona jinsi mlivyo pendeza yaani kama wifi vile wai kaka tutauza mbuzi wa tajiri ili kukamilisha mahari.

Anonymous said...

Kaka naona jinsi mlivyo pendeza yaani kama wifi vile wai kaka tutauza mbuzi wa tajiri ili kukamilisha mahari.

Anonymous said...

It`s true mmpendezana sana kaka damu ikichanganyika yani mtoto atatoka bomba vp changamka kijua ndo hiki........

Anonymous said...

Just take your time Kanumba,the beautiful ones are not yet born.....I love your films,keep the radiance.





Maryam,Germany.

Anonymous said...

WAEGO UCKUBALI KAKA MZUNGU KITU GAN KWANZA UYO NI MZEE

DoroBiku said...

Yaani Kanumba "The Great" nakuonea wivu sana, yaani huyo dada anakonga moyo wangu jinsi anavyoigiza katika "Sex and the City" kati ya wote wanne. Hongera kwa ubalozi wako. Natamani ningefahamu kuwa mlikuwa na shuguhli pale makumbusho ningefika!! Hongera kwa Kazi nzuri

Anonymous said...

watanzani adi leo ushamba bdo ujatutoka wpi mzungu anakotolewa mali wtu wpo kikazi nyinyi kuoa kuchanganya rangi yametokea wpi mzungu mmemuona kma nani mungewajua hao wtu ata musingeshoboka ivyo poleni bcz mupo mbli nao ugaibuni apa

Anonymous said...

mmh hongera kaka kwa kuwa baloz nimependa jinsi unavyojihusisha na mambo ya kijamii by the way mtumie huyo mzungu akupe maujanja ya vip wao wanafanya kazi zao za uigizaj na kuwa bora zaid pia mlipendeza sana