Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Dec 26, 2011

THE GREAT NA X MASS...

Mara baada ya kutoka kanisani niliandaa chakula nyumbani kwangu,nikachoma nyama ya mbuzi na kuku,nikaandaa vinywaji,basi nikawaarika ndugu na jamaa wachache tu waje nyumbani tufurahi xmass hii.Kila mtu nilihakikisha anapata kinywaji anachopenda hata wanywaji wa pombe nao walipata wanachokipenda.Maandiko yanasema tazama ilivyo vyema kwa ndugu kukaa pamoja na kufurahi.
Sebuleni kwangu ndio kulikuwa counter...ahhahah
Walikuepo wazee wa konyagi,wazee wa nyama choma ahahahh
Story za hapa na pale zilikuepo.
Kubadilishana mawazo.
The great na bbm?kha?

Watu wakafurahi nami nikafurahi maana nimekuwa busy sana mara shooting,mara safari nje ya nchi,mara safari za Startimes,mara safari za Oxfam,mara busy ofisini nakosa mda wa kujumuika hivi nyumbani,hivyo x mass hii nikaimaliza hivi.Zaidi ya yote sifa na utukufu nikamrudishia GEHOVA EBENEZER,GEHOVA ELISHADAI,GEHOVA SHAMA.......EMMANUEL(Mungu pamoja nasi)

14 comments:

MCHONGO TV said...

Inapendeza sana kaka,wote tulifurahi sana tunashukuru kwa ukarimu na upendo wako.
Be Blessed sana!

Anonymous said...

umefanya vizuri kanumba ubarikiwe na upendo huo ni kwelikula pamoja na ndugu na marafiki unazidi kubarikiwa kanumba nyumba yako nzuri ubarikiwe zaidi na zaidi

Anonymous said...

K mbona huwa huectii nyumbani kwako wakat pako pouwa sana jaman???

Anonymous said...

safii saana kaka yangu mpendwa kanumba ndiomana nakupenda always.Mungu akuzidishie baraka tele.kwakweli sikunikija dar lazima nikutafute unanigusa saana unavyoishi na upendo wako kwa watu wengine ur my role models,kama kawaida nimimi mdada wako sweden nikweli sikunikija hm nitakucheki unikumbuke tuu mdada wa sweden nikikupigia simu ujue nimimi.barikiwa saana kaka.ila bado ujalifanyia kazi swali langu kuwaupatane na rafiki yako b4 this ending year please.baraaka zinamiminika mpaka utashangaa utapata kazi namikataba kibao mpaka utaikimbia chezea bwana Yesu wewee.

Anonymous said...

Watasonyaje? Walisema umenunua gari la mamilioni wakafikiri huna mahali pazuri pa kulazia mbavu zako.

Anonymous said...

Safi sana, ila kama una maanisha Mungu, ni Jehova na sio Gehova

Anonymous said...

NYUMBA INATAKA MKE SASA!!

Anonymous said...

Hii ilikuwa kifamilia zaidi, nimependa.......Siyo lazima kila siku uwe na mashoste

ak47 said...

Kanumba km finally umegundua mademu wenye majina hawafai kuwa wapenzi NAKUPA BIG SN kila siku mi nilikuwa nakoment humu tafuta mwanamke asie na jina na asiependa publicity hata km atatoka na Kanumba. Yani SOMEONE WITH NO NAME km vile mchumba wa Ndauka watu tumemjua baada ya kutambulishwa jamaa hata mbele za watu hana shauzi hata km yupo na kifaa km kile.

Anonymous said...

Kanumba punguza kulalamika km ushajua mademu wenye majina hawafai zen chill utapata tu. Nakuombea upate ambae hata kupenda kwasababu we ni Kanumba akupende kwa zati,amjue Mungu,muogopa magazeti, na asiwe hata na ushoga na mademu wenye kupenda publicity.

Anonymous said...

you are so great kanumba,Mungu akuzidishie nguvu.

Anonymous said...

Kanumba Kanumba..u r a great man...Mungu akushushie baraka zake..u deserve a better half kanumba...Mungu akupe mke mwema na mrembo pia maana u r just too good..just good kanumba..hii ni sala yangu kubwa kwako siku zote..

daizy said...

hongera bro zidisha upendo zaidi na muombe mungu akupatie mke mwema

Milka Richard said...

Hongera sna kaka,ni vizur cku za ckukuu kukaa na familia na ndugu na marafik mkisherekea pamoja,barikiwa sna.Mm ni mpenz wa kaz zako sna kanumba.na ninakuombea kila day upate mafanikio zaid ya hayo.Ila ucache kumshukuru Mungu,tatizo linaloniumiza ni kuhusu ww na swahiba wako Ray.Ondoen hizo tofaut muanze mwaka vizur jamani,haipendezi????Msiwape wa2 nafas ya kusema.Wengine co wema?watatumia kutofautiana kwenu ili wazidi kubomoa zaidi.NAOMBA MUNGU AWAONGOZE KTK HILO NA MPATE SULUHU.