Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jan 20, 2011

THE GREAT IN NEW YORK....

Leo nimetembelea New york city kununua vifaa vya production katika kampuni yangu...nimetembelea duka moja kubwa na maarufu kwa vifaa vyote vya movie production na sound linaloitwa B&H. Nikitizama taa nzuri kwa production

Nikiwa makini kuchagua ili mashabiki wangu wa ukweli niwe nawapa vitu vyenye quality

Hapa ni sehemu za BOOM MIC pesa yako tu hapo kuna kila aina ya mic kwa ajili ya production napo nilichukua mojawapo ili sauti iwe nzuri katika movie zangu.

Hizi husaidia kuzuia upepo wakati wa shooting

Duka hili lina kila kitu hadi drums,hapa nikijaribu kidogo ili siku nikija kuwa mwanamziki nipite tena hapa.

Vinanda na spika zake vipo







Japo camera tayari ninayo tena nzuri tu ila nilipita hapa sehemu zinapouzwa camera kuosha macho kidogo kwa sababu sikuitaji kitu hapa.



Crain zipo za aina mbalimbali

Duka lenyewe linavyoonekana kwa nje katika mitaa ya NEW YORK.

Kwa vile vifaa nilivyoweza kubeba kwa mikono nilibeba vingine nilipakia,hii ni kuonesha kuwa kwa mwaka 2011 mashabiki wangu nimejipanga vizuri kukonga nyoyo..

8 comments:

Anonymous said...

kwani bwana kaka jacket na raba unavyo hivyo tuuu? jaribu kubadilika kaka ,hujapata designer mzuri,

Anonymous said...

Hongera bwana tunasubiri hizo filam zako mpya

Anonymous said...

hongera kanumba mungu akuzidishie uko juu kijana na kweli kipaji cha kuiimba unacho uliposema siku ukija kuwa mwanamziki nimenda hiyo aidia unapendeza sana kuwa mwanamziki

Anonymous said...

Kaka babu kubwa naona unacheki mambo. tafuta sound recorder zipo nying sana brand tofauti na bei tofauti na features tofauti ila tafuta moja itakusaidia sana kuboresha ubora wa sound kweye filamu zako. unaweza kuwa na camera bora sana kama RED 1, 16mm, 35mm etc ila kama ubora wa sauti ni poor filamu yako itakuwa crap. unaweza kuwa unatumia camera ya simu yenye pixels 5 na sound ni ya ubora wa juu.
Nakuja bongo mwezi wa nne, nikipata wakati nawe ukiwa free tunaweza kuonana. Haya ni maoni yangu tu ambayo yanatokana na professional yangu ya filmmaking na sound design for screening.

Asante Kitojo (UK)

Anonymous said...

Hi Mr "SK" kama ninavyopenda kukuita....Nimefurahi sana kusikia kuwa upo ndani Jiji la MAMA...nakutakia mapumnziko mema na shopping njema...."GOD BLESS YOU !


Wellcome to Denmark!

Thanx,
A.Hermis (TWALIB)
in Copenhagen DK.

Anonymous said...

mwenzangu hata mie nilimwambia vipi jacket kaka ama limeganda?

Grm Production said...

Kaka hongera sana na safi sana . Hayo ndio mageuzi tunayo yaitaji 2011. Vipi kuna ka Jagermeister manake hiyo baridi sio mchezo

Anonymous said...

Binadam bwana sasa ulitaka awe na majacket kumi kwani kahamia huko?acha ushamba ww watu hatuangalii mavazi tunaangalia mafanikio acha roho mbaya..shwaiiiiiiiiin..