Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jan 28, 2011

ZIARA YANGU HOLLYWOOD(LOS ANGELES)

Nimetembelea Hollywood hapa UNIVERSAL STUDIOS kuona mambo mbalimbali ya filamu za hapa hollywood,hii inakuwa mara yangu ya pili kufika hapa.


Hawa ni wasanii walioko maeneo haya ya UNIVERSAL STUDIOS.





Hollywood ndio hiyo,,,


Hii ni SOUND STAGE 12,ndiko kunakorekodiwa tv shows au scene za ndani katika movie


Nikishangaa kwa 3D namna alivyotengenezwa yule nyani wa KING KONG


Kwa wale wanaojua mambo ya blue au green screen mnaelewa kazi yake hiyo,hapo unaweza kushoot alafu katika editing ukawekwa sehemu yoyote.


katika movie movie wengi hushangaa magari yanawezaje kupaa na kulipuka?basi huu ndio utaalamu wao.hapa kabla


Director akisema action basi hali huwa hivi...





kisha hurudishwa sehemu yake kwa namna hii


Jinsi wanavyotengeneza mvua


Bomba hili linatoa maji kwa juu kama mvua ambapo


Jinsi wanavyotengeneza mafuriko ya mvua,hufungulia mabomba makubwa pembeni ambayo huleta maji kwa kasi kama unavyoona

Maji yakipungua na kuingia katika mitaro ya kutengenezwa

Hii ni mfano wa meli ambazo hutumiwa shooting na baadae katika editing na special effect hufanya meli kuonekana kubwa kulingana na saizi waliyokusudia,hili unaweza kuliona katika TITANIC MOVIE

Jinsi ya kutengeneza maporomoko ni kama unavyoona hayo yote yanaendeshwa na umeme

9 comments:

Anonymous said...

Bip up Kanumba.... Keep it up! Uko juuu...

Anonymous said...

picha nzuri tunaenjoy tuma zingine zaidi.hii ndo inatufanya tutembelee blog yako kwa sasa

Anonymous said...

Duh! asante kaka kwa kushare nasi big up sana tuuuuuuuuuuuu

gee said...

hongera sana kanumba hope umejifunza mambo mengi now ukirudi picha zako zote lazima zitishe ndugu yangu, hongera sana sana, ki ukweli mimi nakukubali wangu, unapiga mzigo. endelea kufanya mambo na mungu atakubariki pia jaribu kusaidia wale ambao hawajiwezi sio kwa kuigiza tu hata watu wakawaida katika jamii.

Anonymous said...

Mwe kwa wenzetu kunamaajabu, bora umetupa mwanga kidogo, maaana ilikuwa giza kikubwa kaka.

Glory said...

kazi nzuri kaka, asante kwa kutujali wateja wako kwa kuboresha kazi zako. be blessed. Glory

misswhite said...

Hongera sana kaka kanumba kwa michezo yako mizuri kwani inaelimisha na kufurahisha, pia nataka nikwambie hiyo background yako ibadilishe kwani inasababisha blog kuwa very slow

rachel kayuni said...

sijawahi ku comment kwako kaka yangu leo nacomment. kiukweli nimependa sana hizi picha zimenifanya ijione kama na mimi nipo holywood lakini kikubwa ni kwamba nimepata elimu , umenitoa tongo tongo sana hasa kwenye green screen. thanx

Anonymous said...

aisee ni nomaa umetuletea kitu kizuri sna kanumbaaa i wish wanaoekti filamu za kupigana wabongo wangeenda huko kuona wenzao wanavyofanyaa ingewasidia sana.


meggie impostra