Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Jun 12, 2010

THE GREAT NA LISA JENSEN KATIKA SCENE ZA SHULENI NDANI YA ''MORE THAN PAIN''

Wanafunzi haoooooooo

Hili kosa sijui tutali solve vipi?

Lisa akiwaza mbona tumetolewa gafla darasani?bila shaka ndio nafukuzwa shule...

Vijana wangu wa kazi toka GRM PRODUCTION wakiandaa vifaa tayari kwa shooting

Back shot..

Lusubiro na Hamidu wakiitendea haki stead cam yaani camera ya kuvaa kifuani ii uweze kutembea nayo

Headmaster akitoa speech kali..

Wakati fulani huwa naisaidia crew yangu kama unavyoona maana production huitaji ushirikiano wa dhati ili kazi iwe bora zaidi

Tukisoma matokeo hapo ni Seth,Tino na mimi

Lisa akitoloka shule kwenda kwa.....


mmmmh mapenzi shuleniiiii ni hatari..

kwa pamojaaa wanafunziii

Darasani Tino ndie anayeongoza kwa kupiga kelele na utundu.....

muda wa kantini huu kila mwanafunzi anatabasamu saana

8 comments:

Ney said...

Hongera kaka kwa kazi nzuri,
kama wapenz wa movie zako, tulikuwa tunakushauri, unaonaje uresearch kuhusu watu mashuhuri kama mkwawa na utoe story zao kwenye nyanja ya mapenz (mfano yeye alikuwa na wake wengi), ushujaa wake na mpaka alivojiua..
Kuna story ya kufikirika yenye kuelezea vita vya kagera (kutoka ktabu cha zawadi ya ushindi cha amandina lihamba..) na hata story ya karume na ushujaa wake wa kuletea mapinduz zanzibar mpk alivouwawa... Na nyngine nyingi..,Tena kwa story za ktaifa kama hzi unaweza kutafutia fund na wafadhili.. Mkatunza historia kwa njia ya filamu kama wafanyavyo wenzetu.

Anonymous said...

sio siri nimeanza kuipenda kabla haijakamilika, bila shaka itakuwa kali ile mbaya.

Anonymous said...

EE BWANA KANUMBA KWANZA NAANZA KWA KUKUPA PONGEZI NYINGI SANA KWA KAZI NZURI NA MAFANIKIO ULIYOPATA KWENYE ANGA LA SANAA YA MAIGIZO NDANI NA NJE YA NCHI YA TANZANIA.UKIACHILIA MBALI MAFANIKO PIA MIMI KAMA MSHABIKI WAKO MKUBWA NA KAMA MTANZANIA NAPENDA KUTOA YANGU MACHACHE MAONI ILI KAMA YATAKUFAA BASI YASAIDIE KUBORESHA KAZI YAKO NA MAFANIO ZAIDI KWA UJUMLA. KWA KWELI UKIANGALIA PICHA ZAKO AU MIE NIITE MOVE AMBAZO UMEKUWA UKIZITOA NI CHACHE SANA ZINAZUNGUMZIA MAISHA HALISI YA MTANZANIA HASWA WATANZANIA WANOISHI VIJIJINI NINGESHAURI UJARIBU KUFANYA SHUTING MFANO MOROGORO KILOSA AU TURIANI NA UJARIBU KUZUNGUMZIA NA KUONESHA TASWIRA HALISI YA MOROGORO NA MAZINGIRA YAKE PAMOJA NA MAMBO MENGINE MENGI UTAKAYOYAONA YANAFAA KUMULIKWA. SI MORO TU NA MIKOA MINGINE AMBAYO SIJAITAJA HAPO.HII ITASAIDA SANA KUPATA MASHABIKI WENGI SANA NDANI NA NJE YA NCHI KWANI KILA MTU ANAPENDA KUFAHAMU HALI HALISI ILIYOPO HUKO MIKOANI.NYINGINE PIA MOVE ZAKO NYINGI ZINAONESHA TASWIRA (MAISHA) YA KIFAHARI TOFAUTI NA WATANZANIA WALIO WENGI UKIANGALIA NYUMBA, MAGARI NAMAVAZI HAYAMULIKI MTANZANIA HALISI AU WALIO WENGI. NAJUA UKWELI KILA MTU ANAWEZA KUSEMA KILE ANAONA KINAFAA ILA KWA UPANDE WANGU MIE NIMEJARIBU KUTOA ANGALIZO TU. DAN MDAU FINLAND

Anonymous said...

Mambo ni aje Kanumba..mimi ni mpenzi sana sana wa movie zako na huwaga nakukubali kwa asilimia moja..kwani najua wewe una kipaji na unajua kuigiza tofauti na waigizaji wengi wa kwetu ambao huwaga wanalazimisha...nakushauri tu ili na wewe usipotoke jitahidi kuweka uhalisia wa filamu mtu kama tino kwa umri na appearence yake hakutakiwa kuwa mwanafuzi inaondoa uhalisia kabisa kwa wewe sawa..ungetafuta msanii yoyote ambae ana umbo au sura ya kiuanafuzi wa sekondari tino anaonekana amezeeka na hio poda aliyopaka ndio anazidi kuwa kituko.Mimi nimesomea mambo hayo na nina uzoefu nayo.Wasanii wengi wa bongo wanashindwa kwenye kuleta uhalisia wewe kidogo afadhali ila kwenye hili unaanza kuboa.Jali kazi zaidi kuliko kuijali marafiki wauze sura kwenye movie..

Swabra said...

aisee kanumba nakukubali sana hiyo move yako itakuwa kiboko nimeikubali vibaya mno! Mungu akujalie na akutie nguvu katika kilajambo ambalo unalo likusudia
aaaamini

Unknown said...

itakuwa bonge la picha .. Tafadhali toa mapema mdua naingoja kwa hamu.. big up kanumba..

ESM said...

dah brother sure ua great men, ktk issue za filamu nimekuwa nikifwatilia kazi zako kwa karibu mno, we ni mbunifu vya kutosha,umeimarisha nidhamu ktk shughuli zako. kitu ambacho ningependa kukushauri jaribu kuwahamasisha wenzako kuwa wavae uhusika vizuri kwa mfano mtu anaweza kuzungumza jambo la huzuni lakin uso wake unaonyesha ni m2 mwenye furaha au unamuona m2 anaigiza huku anafikiria maneno ya kwenye script. ni hayo 2 brther.

Unknown said...

HONGERA SANA KAKA.NAKUOMBEA UPATE MTOTO WA KUKURIDHI FANI YAKO.