Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Dec 22, 2010

SAFARI YETU KUELEKEA OFISINI KWA WAZIRI WA UTAMADUNI BUKAVU.

Tukiwa Bukavu tulipata mwaliko kumtembelea waziri wa utamaduni Bukavu,hivyo msafara mzima ulikuwa hivi. Baadhi ya mashabiki waliokuwa wakituona waliyazonga magari tuliyomo hivyo kusababisha foleni kubwa barabarani kama unavyoona.

Safari ikawa ngumu kidogo maana mashabiki walitaka kutuona na tuwasalimu kidogo nasi ikabidi tufanye hivyo kama unavyoona Jeniffa akiwa juu ya Gari kuwaridhisha mashabiki.Kwa upande mwingine Jenifa amekuwa kivutio kikubwa sana kwa watu na amejizolea mashabiki wengi sana Congo.

Tukiingia ofisini kwa Waziri

Nami nikiingia

Aunty akipokelewa mlangoni

Tukibadilishana mawili matatu na mheshimiwa mbele yetu aliyekaa mwenye suti nyeusi

Mheshimiwa aliomba tusaini katika kitabu chake cha wageni maalumu waliowahi kumtembelea ofisini kwake nasi tukafanya hivyo.

Sehemu ya ujumbe wangu niliokuwa nikiandika baada ya kusaini

Zamu ya swahiba kusaini

zamu ya Irene Uwoya

Johari nae alifata

Aunty Ezeckiel akafata

Mwisho alimalizia Jeniffa.

Picha ya pamoja na mheshimiwa baada ya maongezi na kusaini

Nje ya ofisi ya mheshimiwa waziri mashabiki walijaa kwa wingi wakitusubiri kwa hamu tutoke ili watuone tena.

1 comment:

Anonymous said...

kwakweli mambo ambayo mliyoyafanya inchini congo inaonesha waziwazi kuwa nyinyi ni watu muhim sanaa katika jamii kwa hiyo napenda kusema kwamba kazaneni na kazi na vile vile mungu azidi kuwabariki sanaaaa nyote kwa jumla