Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

Mar 30, 2010

KANUMBA THE GREAT FILMS mambo bado yanapikwa leo ilikuwa ni siku ya kupiga scene za MONTAGE ktk movie

Cameraman wangu kutoka GRM PRODUCTION Lusubiro Mwanguku Akiwasili location tayari kwa kuanza ku set vifaa ili shooting ianze.

Huyu dada ni shabiki yetu mkubwa na mdau toka UK alifurai sana kukutana nasi maeneo hayo hivyo akaomba kupiga nasi picha mimi na Aunty lakini pia tulimualika katika set ashuhudie jinsi tunavyorekodi

Kazi imeshaanza bila kupoteza mda.

mmmmmmh ni acting tu jamani na si vinginevyo katika kupata montage nzuri

Unaweza kudhani ni BRAD PITTY na ANJELINA JOLIE ahhahahahah

Duh?Gwantwa utaniangusha bwana

Jamani katika movie hii nimejiandaa vizuri sina haraka na sikurupuki kama kawaida yangu ni kubring the best and great

Sio siri kwa sasa kiwango cha Aunty Ezekiel kimeongezeka zaidi mbali na kuwa directed pia kutumia script lakini yeye kama msanii ana vitu vyake vya ziada ambavyo kwa hakika vimeongeza utamu wa movie

Kazi ikiendelea sawia

The great na Gwantwa katika mapozi kuntu

Baharini tukiendesha pikipiki ya majini ni montage mojawapo katika movie hii

Tukipiga masafa huku camera imefungwa katika crain ikitufata

Kuna wakati Aunty alikuwa muoga pindi nilipokuwa nikikimbiza pikipiki ikabidi nimshushe kwanza nirekodi peke yangu huku nikiwa katika spidi kali katikati ya bahari

Maya akimfungua boya Aunty mara baada ya kumaliza kurekodi montages

Aunty Gwantwa akifungwa boya na kupewa maelekezo jinsi ya kulitumia kabla ya kuanza kazi.

14 comments:

Anonymous said...

Loh Gwantwa unadatishaaaaa.
hahahahaah kama Brad and Angelie umenifurahisha kweli.


disminder.

Anonymous said...

kaka big up mimi sana sitaki kumponda fulani anayetoa filamu fulani kila weekend mimi kwa upande wangu nakubali kazi yako sana kusema la kweli huko juu sana kaka cha msingi ni kukaza buti tu

Anonymous said...

duh we Kanumba huko kuigiza gani na huyo aunt? mhhhh nyie lazima mtakuwa wapenzi tu , hahaaaaaaaa

Majoy said...

duuuh ama kwa hakika hii movie itaku poa sana,naingoja kwa hamu sana hii ni dhambi kuikosa jamani!!!!!!

Anonymous said...

Ndugu yangu kanumba una moyo sana, hapo umeondoka bila bila kweli? Du!! ndio maana hamuwezi kuoa, ni movie lakini burudani mnapata ya kutosha. Anyway nakutakia kila heri maana movie ndio kazi yako na maisha yako yanasonga mbele kwa hiyo kazi. Mdau EU

pac said...

mkubwa imetulia hiyo ki2 hapo beach..m2kama una mkeo anaigiza halafu hujui sanaaa..inakuwa kaazi kweli kweli..

Lakini veve mwanambati..suruali beach kama haiko mwake vile mkubwa???

Wewe ungejiachia na mavi2 ya vitu laini short hiviiiiii

Anonymous said...

hata kama ni action ila nyie naona kama vile mnafanya kweli haiwezekani aunt akupanulie mapaja hivyo afu nawe unayshika utafikiri ndo mpo chumbani nyie mnafanyana kweli maan aunt alivyo kamekaa kikahaba zaidi duh hata amfundishi vitu vya maana sana mnafundisha watu wafanya ujinga, najua utaibania hii coment lakini ujumbe umekufikia pls itoe hewani

Albert said...

Ndiyo Kanumba, endelea na kutuandalia vitu vilivyo vizuri na vitamu kabisa. Watu wa Australia tunasubiri kwa hamu chochote utakachotupa kwani kiwango chango cha ku act ni cha hali ya juu kabisa. Lakini uwe makini sana na Aunty kwani anavyokamua ni zaidi ya kipaji cha kawaida. I mean ni actress mzuri sana, namuamini sana, na umpe habari kwamba nitamshirikisha kwenye movies ambazo tuko tunaziandaa hapa Australia.
Keep it up Bro. Kanumba.
Albery
Australia

Anonymous said...

Halafu wakiulizwa eti wanasema hapo hakuwa kanumba na aunt, hapo alikuwa gwantwa na nanihii uwongo mtupu hata kina brad na angeline walikutana kwenye acting ndio wakaoana.

kokusimah said...

wow ngoja niwe nasubila, manake natamani niipakue haijaiva. Kazi njema kakangu, napenda kazi zako. Wasanii wabongo mmepanda siyo siri. kila la kheri.

Anonymous said...

hivi hamjashtukia kwanini huyu mwanambati alivaa jinsi hapo ufukweni?yani kwa hizo scene na hicho kitoto kilivyo aliogopa 'babu juma'wake 'angeonyesha ushirikiano'afu ingekuwa soo!

Anonymous said...

Kanumba polepole huu ni mwezi wa nne tusije sikia tunapata mjomba baada ya miezi tisa. maana huyo Gwantwa anavyokaa kaa si utani atawavutia wengi! wanaopenda nanihii!!!

Anonymous said...

Sasa Kanumba hii picha utaturuhusu tuangalie na watoto wetu? au hizi sehemu za Gwantwa na Wewe katika mambo yasiyompendeza Mungu utaziondoa? Maana siamini watoto wa Kiswahili wakiangalia hivyo tu Kesho wasijaribu hayo mapigo. Mifano tunayo Maana wakimuona JOHN CENA tu kesho wanajitia wababe. Ushauri: Andika juu ya Gamba Watoto hawaruhusiwi!!!! Kizito

capt steve said...

haya bwana naona mambo si mambo hahahaha