Star Times

Star Times

Mercy Beauty Parlour

Mercy Beauty Parlour

May 31, 2010

THE GREAT NA ADOLPHE DOMINGUEZ WA WENGE MUSICA

The great niliamua kumtembelea hotelini alipofikia mwanamziki mkongwe kutoka CONGO ambae pia ni muasisi wa wenge musica bcbg kabla ya kujiengua na kuunda kundi lake la wenge tonya tonya,nikaamua kumtoa kidogo kwenda sehemu kadhaa kama... Hapa ilikuwa katika studio za GRM PRODUCTION tukipiga picha za kumbukumbu ambapo pia video camera ilikuwa ikishoot ambayo nayo nilimpatia aondoke nayo.


Hapa akiwa na mkurugenzi wa GRM PRODUCTION Nd.G.Makupa ambae zoezo zima la picha aliliongoza yeye hapo studio.

Hapa nikimkabithi zawadi ya simu mpya kama kumbukumbu pindi afikapo kwao

mdau,adolphe,the great na G.Makupa kwa pamoja baada ya kumpatia zawadi ya simu Adolphe

Hapa nikimkabithi zawadi ya movie yangu mpya inayosumbua kisawaswa THIS IS IT 1&2 ambayo aliomba maana kwao bado haijafika

kwa pamoja tukiimba wimbo wake wa VOYAGE alioutunga na kuimba zamani akiwa na wenge bcbg akiwa na JB MPIANA,BLAISE BULA,WERRASON,AIMELLA,ALLAIN MPELLA,ALLAN MAKABA,nk.

aliniomba kabla ya kumkabithi movie zangu nisaini kwanza nami nikafanya hivyo

Nae pia baada ya kumrudisha hotelini alinipa zawadi ya albam yake mpya aliyoimba na KOFFI OLOMIDE(audio na dvd)inayoitwa SUSPENSION

Hii ni moja ya picha tulizopiga na kuzikuza na kutoa picha kubwa2 ambazo kwa upande wake alisema anaenda kupamba nyumbani kwake lakini mimi nilisema ntaweka ofisini kwangu ambapo nilimpitisha akapaona.

7 comments:

Anonymous said...

Kuna picha nimeiona kule kwa Jide,aisee nimecheka sana lile pozi sijui lilikuwa lakuwakwepa vijana wa shigongo? au? by the way mlipendeza sana na Sylivia wako.

Anonymous said...

Kuna picha nimeiona kule kwa Jide,aisee nimecheka sana lile pozi sijui lilikuwa lakuwakwepa vijana wa shigongo? au? by the way mlipendeza sana na Sylivia wako.

Anonymous said...

hivi ile white maria tayari kutoka coz ulitupromise june,yani nina hamu nayo.i cant wait to see kanumba and wema again!

Anonymous said...

safi sana dogo

afrolife said...

Steve, sanaa inasambaa sana kwa kweli; last month i was in congo-kinshasa (avenue nguema),nikiwa kwa hoteli nilishangaa sana kuona movies za kibongo zikiwa aired karibu kila siku kwenye baadhi ya TVs kama Mirrador TV, Congo Digital, HD Congo etc. Ningewashauri 1: Muwe mnatoa versions zenye subtitles za french (wakongo wengi hawajui English wala Kiswahili). 2: Mfanye close monitoring ya distribution chain yenu kwani soko la movies za bongo laelekea ni kubwa sana congo na wajanja wachache waweza kuwa wanawaibia.
kazi njema!!

Anonymous said...

vp mzee wa the great,
mm naiulizia ile filam ya white maria with wema imetoka tayari?
na ww anonymous wa may 31,2010 2:12 unaongelea nn silvia na kanumba kukwepa shigongo? vp kama wapenzi ilikuwa wema so silvia maneno tu ya watu, kwanza hata hawaendani. ongea mambo ya maanda bwana, kanumba umependeza na hy mwanamziki, kuja kipaji bwana achana na madem fanya kazi watu wanapenda.
mdau.

Hadj Drogba "mwana chelsea" said...

Aah kaka umenikumbusha mbaaaaali kuniwekea Papaa ADOLFE Katika blog yako,mimi ni big big fun wa wengee musica iliyokuwa imeshiba na kusheheni vijana(Wakati huo)wazuri watanashati chini ya Le Souveree premiee mukulu wa bakula le gra le dee carithmatike genarasioo de la music congolee huyo si mwingine bali ni MPIANA TSHITUKA A.K.A.JIBEE MPIANA,Akiwa na kina Huyo Adolphe,Sele Bulla a.k.a.Blaize Bulla,Werrason a.k.a. le Gra de la foreee,Alee "Prince" Makaba,repa(atalaku)namba moja barani afrika ROBERTO EKOKOTA,Then baadae kwenye rapu akaja kijana mmoja mdogo wakati huo Yombo Lumbu a.k.a.TUTU KALUDJI LE NAMBARI ONE,Kina EMELIA LYASE,Alee mpella
"Afande",kwenye magitaa ukiacha prince alee makaba kulikuwa na mtu anaitwa Burkina Faso "fasolafasola",(solo),Pia alikuwapo muanzilishi "le foundee" na pia mwenye alitoa hilo jina la wenge huyu si mwingine bali ni DIDIER MASELLA(Bass),Ficaree Mwamba (rithym),kanumba acha bwana those were the days kaka,hebu jaribu kutumia ushawishi wako hawa jamaa japo wakutane wafanye album moja tu kwa mwaka.Naipenda wenge nampenda sana JB MPIANA Kaka aah...,Pamoja na voyage ya huyo Adolphe pia wimbo wake mungine niupendao ni ule wa "NO COMMENT SHENGEN" Hebu usikilize halafu utaniambia kaka